MWAJOMBENEWS


Hii ni blog mpya inayo milikiwa na EVANS SOMBE; inayokuletea habari mpya na za uhakika punde tu zinapotokea pia waweza kupakua nyimbo na video bure kabisa.Endelea kuwa mjanja kwa kutembelea blog yetu kwa habari motomoto.


Breaking

Monday, June 19, 2017

HISTORIA YA SARAFU TANZANIA



Kabla ya mwaka 1884, nchi yetu ilikuwa inatumia sarafu moja ya Riyal iliyokuwa imetolewa na Sultan wa Zanzibar chini ya Sultani wa Oman. Sarafu za Riyal zilikuwa kama ifuatavyo


Riyal


[​IMG]


[​IMG]


[​IMG]

Baada ya 1884, Zanzibar ilitumia sarafu za aina tatu kwa mpigo. Sarafu ya kwanza ilijulikana kama Maria Theresa Thaler iliyotolewa Italy, ilikuwa na sura ifuatayo.


Maria Theresa Saler


[​IMG]

Sarafu ya pili ilikuwa ni rupia ya kihindi pamoja na visehemu vyake ambavyo vilikuwa vingi kidogo. Sehemu kubwa za rupia zilikuwa ni Anna, pice , robo rupia na nusu rupia:


1 Anna

[​IMG]


1/4 rupee


[​IMG]


1/2 rupee

[​IMG]

1 rupee


[​IMG]


Pesa hizi zilikuwa ngumu sana hasa kwa vile Anna ilikuwa na vipande vingine kama 1/12 ya Anna, 1/6 ya Anna, 1/4 ya Anna na kadhalika. Sikuweka picha za vipande hivi ingawa ninavyo.


Sarafu ya tatu ilikuwa inajulikana kama Zanzibari Rupee ambao kimsingi ilikuwa sawa na rupee ya kiingereza iliyokuwa ikutumika Kenya na Uganda. Sikupata picha yake.


Kwa upande wa bara, kuanzia mwaka 1884 ilikuwa inatumia Rupie za kijerumani. Rupie moja ilikuwa imegawanyika katika pesa 64. Neno la kiswahili "pesa" linatokana na sehemu hii ya rupie.


Pesa 1

[​IMG]


Rupie 1

[​IMG]


Mwaka 1891 ziliongezwa sarafu za robo rupie na za nusu rupie kama ifuatavyo.


1/4 rupie

[​IMG]


1/2 rupie

[​IMG]


Ilipofika mwaka 1893 ikaongezwa sarafu ya rupie 2 iliyoonekana kama ifuatavyo


2 Rupee

[​IMG]


Sarafu zote hizo ziliendelea kutumika hadi mwaka 1904 ambapo sarafu ya rupie iligawanywa katika vipande mia moja (decimalization), kila kipande kikijulikana kama "heller." Neno la kiswahili "hela" limetokana na mgawanyo huo. Sarafu za

nusu heller na heller moja zilitolewa wakati huo zikiwa na sura zifuatazo.


1/2 heller

[​IMG]


1 heller

[​IMG]


Kipindi hicho, sarafu za robo rupie, nusu rupie, na rupie 1 zilitolewa upya zikiwa na sura zifuatazo:


1/4 rupie

[​IMG]


1/2 rupie

[​IMG]


1 rupie

[​IMG]


Mwaka 1908, serikali iliamua kuongeza idadi ya sarafu kwa kuingiza sarafu ya heller 5 na heller kumi zilizokuwa na sura zifuatazo.


5 heller

[​IMG]


10 heller

[​IMG]


Hata hivyo, ilipofika mwaka 1913 sarafu ya heller 5 ilibadilishwa sura na kuwa kama ifuatavyo


5 heller

[​IMG]


Sarafu hizi ziliendelea kutumika hadi vita ya kwanza ya dunia ilipoanza mwaka 1916. Mwaka huo serikali ilitoa sarafu ambazo hazikuwa zimetengenezwa kwa ufundi kabisa. Sarafu zilizotolewa wakati huo zilikuwa zile za heller 5, heller 20 na rupie 15. Sarafu za heller 5 na heller 20 zilikuwa na sura ifuatayo.


heller 5

[​IMG]


heller 20

[​IMG]


Sarafu ya rupie 15 ilikuwa ya dhahabu, ilijulikana kama "Tabora Pound." Ni kati ya sarafu ambazo zilikuwa ghali sana katika historia ya nchi. Kwa bahati mbaya siyo sarafu nyingi zilizoingia kwenye mzunguko kutokana na vita, kwa hiyo nyingi ziliishia kwenye minada ya wakusanya sarafu. Sura yake ilikuwa kama ifuatavyo


rupien 15

[​IMG]


No comments:

Post a Comment