Noti za karatasi zilianza kutumika mwaka 1905 wakati wa utawala wa
mjerumani kwa upande wa bara. Noti hizo zilitolewa katika thamani ya
Rupie 5, 10, 50, 100 na rupie 500 kama ionekanavyo hapa chini.
Noti za
rupie 500 zilikuwa chache sana na sikufanikiwa kupata picha yake
Rupie 5
Rupie 10
Rupie 50
Rupie 100
Kwa upande wa zanzibar, mwaka huo huo wa 1905, noti za Rupee za
kizanzibari zilitolewa katika thamani za Rupee 5, 10, 20, 50, 100 na
rupee 500 pia. Kwa bahati mbaya sikuweza kupata picha zake zote,
naonyesha mfano wa noti za rupee 5 tano tu niliyofanikiwa kupata.
5 Zanzibari rupee
Wakati wa vita ya kwanza ya dunia, serikali ya kijerumani ilitoa noti za
dharura ambazo zilikuwa ni za karatasi ya kawaida kabisa. Noti hizi
zilikuwa katika thamani za Rupie 1, 5, 10, 20, 50 and Rupie 200 ingawa
hizi za Rupie 200 zilikuwa adimu sana na sikufanikiwa kupata picha yake
1 Rupie
5 Rupien
10 Rupien
20 Rupien
50 Rupien
Noti hizi za dharura zilikuwa hafifu sana na wakati mwingine zilikuwa
zinafyatuliwa kwa muhuri tu kama hii hapa chini ya Rupie 1.
Inaelekea kuwa mji wa Tabora ulikuwa na umuhimu wa pili kwa dar es
salaama wakati wa serikali ya kijerumani kwa vile unaonyeshwa katika
Noti zote. Kama mtakumbuka, ile sarafu ya dhahabu ya Rupie 15 ilikuwa
inaitwa "Tabora Pound."
.....INAENDELEA
Baada ya utawala wa kijerumani kuanguka na nchi kuchukuliwa na
waingereza, kwanza nchi ilitumia noti za Rupee za Afrika ya Mashariki na
Rupee za Zanzibar ingawa Rupie za kijerumani pia ziliendelea kutumika.
Kwa upande wa Zanzibar noti ya rupee 1 ilianzishwa mwaka 1920. baadhi
ya noti hizo ni hizi hapa
1 Zanzibari Rupee
1 EA Rupee
5 EA Rupee
10 EA Rupee
Katikati ya mwaka 1920, serikali ya uingereza ilianzishwa sarafu ya
pamoja kwa nchi zote za Afrika ya Mashariki iliyojuliakana kama Florin
ya Afrika ya Mashariki. Noti za Florini zilikuwa katika thamani za
Florin 1, 5, 10, 20, 50, 100 na Florin 500, ambapo noti za kuanzia
Florin 10 na kuendelea juu zilikuwa pia na thamani ya Pound (1, 2, 5, 10
na 50). Kwa vile sarafu hii haikudumu zaidi ya miezi sita, ni noti
chache sana zilizotolewa, mifano ya noti hizo ni kama ifuatavyo
1 EA Florin
5 EA Florin
Mwanzoni mwa mwak 1921, serikali ya kiingereza ilianzisha sarafu ya
pamoja afrika mashariki iliyojulikana kama Shillingi ya Afrika ya
Mashariki na hivyo kuondokana na Florin ya Afrika Mashariki. Shilingi ya
Afrika Mashariki (baadaye nitakuwa naandika kwa kifupi tu kama
Shilling) ilikuwa na thamani ya Shillingi 20 kwa pound moja na ilikuwa
imeegeshwa kwenye pound kiasi kuwa thamani ya Shilling 20 kwa pound
haikubadilika. Noti za Shillingi zilizotolewa wakati huo zilikuwa za
thamani za Shillingi 5, 10, 20, 100, 1000, na Shillingi 10,000. Noti
za Shillingi ishirini na kuendelea juu zilikuwa pia na thamani ya pound
(1, 5, 50). Noti hizi zilikuwa zimeandikwa kwa kiingereza, kiarabu na
kiamhara kinachotumika Ethiopia. Katika utawala wote wa kiingereza,
kulitolewa mitindo miwili tu ya noti hizo. Mtindo wa kwanza ulidumu
kuanzia mwaka 1921 hadi mwaka 1958, ma mtindo wa pili ulidumu kuanzia
mwaka 1958 hadi baada ya uhuru mwaka 1964. Sura ya mbele ya noti zote
ilikuwa ikionyesha mtawala wa himaya ya uingereza. Sura ya nyuma kwa
upande wa noti za mtindo wa kwanza ilikuwa na simba mmoja wa kiume
katika eneo la mlima Kenya. Noti zilizotolewa mara ya kwanza wakati wa
utawala wa Mfalme George wa tano (1910-1936) ni kama ifuatavyo:
5 EA Shilling
10 EA Shilling
20 EA Shilling
100 EA Shilling
1000 EA Shilling
(Picha hii ilipingwa wakati pesa imeshafutwa rasmi kwa kutobolewa matundu; noti halisi haikuwa na matundu hayo)
Kwa thamani ya shillingi na uchumi wa watu wakati huo, ni noti chache
sana zenye thamani ya Shilling 1000 na Shillingi 10,000 ziliingia kwenye
mzunguko, na sikufanikiwa kupata noti ya Shilingi 10,000. Kwa hiyo
ilipofika mwaka 1933, serikali ikaamua kusimaisha matumiz ya noti za
shillingi 1000 ingawa zile za shillingi 10,00 ziliendelea. Wakati wa
utawala mfupi wa Mfalme Edward wa nane mwaka 1936, hazikutolewa noti
zozote. Noti nyingine zilitolewa wakati wa utawala wa mfame George wa
sita (1936-1952), ambapo noti ya Shillingi 1 ilianzishwa. Noti hizo
zilikuwa kama ifuatavyo.
1 EA Shilling
5 EA Shilling
10 EA Shilling
[/
20 EA Shilling
[/
100 EA Shilling
[/
Kutokana na uhadimu wake, sikuweza kupata noti za Shillingi 10,000. Hata
hivyo miaka 11 ndani ya utawala wa mfalme George wa sita, iliamuliwa
kufuta noti hizi za Shillingi 10,000 ambazo zilikuwa hazitumiki sana.
Baada ya kifo cha Mfalme George wa sita mwaka 1952 na binti yake Malkia
Elizabeth wa pili kuchukua usukani noti zilizotolewa zilikuwa zinafanana
na zile zilizokuwapo mwazoni isipokuwa aliondoa noti ya Shillingi 1
kwenye mzunguko.
5 EA Shilling
10 EA Shilling
20 EA Shilling
100 EA Shilling
Thanks
ReplyDeleteThanks brother
Delete