MWAJOMBENEWS


Hii ni blog mpya inayo milikiwa na EVANS SOMBE; inayokuletea habari mpya na za uhakika punde tu zinapotokea pia waweza kupakua nyimbo na video bure kabisa.Endelea kuwa mjanja kwa kutembelea blog yetu kwa habari motomoto.


Breaking

Monday, June 19, 2017

HISTORIA YA FEDHA TANZANIA

Noti za karatasi zilianza kutumika mwaka 1905 wakati wa utawala wa mjerumani kwa upande wa bara. Noti hizo zilitolewa katika thamani ya Rupie 5, 10, 50, 100 na rupie 500 kama ionekanavyo hapa chini.

 Noti za rupie 500 zilikuwa chache sana na sikufanikiwa kupata picha yake


Rupie 5

[​IMG]


Rupie 10

[​IMG]


Rupie 50

[​IMG]


Rupie 100

[​IMG]


Kwa upande wa zanzibar, mwaka huo huo wa 1905, noti za Rupee za kizanzibari zilitolewa katika thamani za Rupee 5, 10, 20, 50, 100 na rupee 500 pia. Kwa bahati mbaya sikuweza kupata picha zake zote, naonyesha mfano wa noti za rupee 5 tano tu niliyofanikiwa kupata.

5 Zanzibari rupee

[​IMG]


Wakati wa vita ya kwanza ya dunia, serikali ya kijerumani ilitoa noti za dharura ambazo zilikuwa ni za karatasi ya kawaida kabisa. Noti hizi zilikuwa katika thamani za Rupie 1, 5, 10, 20, 50 and Rupie 200 ingawa hizi za Rupie 200 zilikuwa adimu sana na sikufanikiwa kupata picha yake

1 Rupie

[​IMG]


5 Rupien

[​IMG]


10 Rupien

[​IMG]


20 Rupien

[​IMG]


50 Rupien

[​IMG]


Noti hizi za dharura zilikuwa hafifu sana na wakati mwingine zilikuwa zinafyatuliwa kwa muhuri tu kama hii hapa chini ya Rupie 1.

[​IMG]


Inaelekea kuwa mji wa Tabora ulikuwa na umuhimu wa pili kwa dar es salaama wakati wa serikali ya kijerumani kwa vile unaonyeshwa katika Noti zote. Kama mtakumbuka, ile sarafu ya dhahabu ya Rupie 15 ilikuwa inaitwa "Tabora Pound."

.....INAENDELEA

 

Kichuguu

Kichuguu Platinum Member

#2

Sep 4, 2007

Joined:Oct 11, 2006

Messages:7,082

Likes Received:545

Trophy Points:280

Baada ya utawala wa kijerumani kuanguka na nchi kuchukuliwa na waingereza, kwanza nchi ilitumia noti za Rupee za Afrika ya Mashariki na Rupee za Zanzibar ingawa Rupie za kijerumani pia ziliendelea kutumika. Kwa upande wa Zanzibar noti ya rupee 1 ilianzishwa mwaka 1920. baadhi ya noti hizo ni hizi hapa

1 Zanzibari Rupee


[​IMG]


1 EA Rupee


[​IMG]


5 EA Rupee


[​IMG]


10 EA Rupee


[​IMG]


Katikati ya mwaka 1920, serikali ya uingereza ilianzishwa sarafu ya pamoja kwa nchi zote za Afrika ya Mashariki iliyojuliakana kama Florin ya Afrika ya Mashariki. Noti za Florini zilikuwa katika thamani za Florin 1, 5, 10, 20, 50, 100 na Florin 500, ambapo noti za kuanzia Florin 10 na kuendelea juu zilikuwa pia na thamani ya Pound (1, 2, 5, 10 na 50). Kwa vile sarafu hii haikudumu zaidi ya miezi sita, ni noti chache sana zilizotolewa, mifano ya noti hizo ni kama ifuatavyo

1 EA Florin

[​IMG]


5 EA Florin

[​IMG]


Mwanzoni mwa mwak 1921, serikali ya kiingereza ilianzisha sarafu ya pamoja afrika mashariki iliyojulikana kama Shillingi ya Afrika ya Mashariki na hivyo kuondokana na Florin ya Afrika Mashariki. Shilingi ya Afrika Mashariki (baadaye nitakuwa naandika kwa kifupi tu kama Shilling) ilikuwa na thamani ya Shillingi 20 kwa pound moja na ilikuwa imeegeshwa kwenye pound kiasi kuwa thamani ya Shilling 20 kwa pound haikubadilika. Noti za Shillingi zilizotolewa wakati huo zilikuwa za thamani za Shillingi 5, 10, 20, 100, 1000, na Shillingi 10,000. Noti za Shillingi ishirini na kuendelea juu zilikuwa pia na thamani ya pound (1, 5, 50). Noti hizi zilikuwa zimeandikwa kwa kiingereza, kiarabu na kiamhara kinachotumika Ethiopia. Katika utawala wote wa kiingereza, kulitolewa mitindo miwili tu ya noti hizo. Mtindo wa kwanza ulidumu kuanzia mwaka 1921 hadi mwaka 1958, ma mtindo wa pili ulidumu kuanzia mwaka 1958 hadi baada ya uhuru mwaka 1964. Sura ya mbele ya noti zote ilikuwa ikionyesha mtawala wa himaya ya uingereza. Sura ya nyuma kwa upande wa noti za mtindo wa kwanza ilikuwa na simba mmoja wa kiume katika eneo la mlima Kenya. Noti zilizotolewa mara ya kwanza wakati wa utawala wa Mfalme George wa tano (1910-1936) ni kama ifuatavyo:

5 EA Shilling

[​IMG]


10 EA Shilling

[​IMG]


20 EA Shilling

[​IMG]


100 EA Shilling

[​IMG]


1000 EA Shilling

[​IMG]

(Picha hii ilipingwa wakati pesa imeshafutwa rasmi kwa kutobolewa matundu; noti halisi haikuwa na matundu hayo)

Kwa thamani ya shillingi na uchumi wa watu wakati huo, ni noti chache sana zenye thamani ya Shilling 1000 na Shillingi 10,000 ziliingia kwenye mzunguko, na sikufanikiwa kupata noti ya Shilingi 10,000. Kwa hiyo ilipofika mwaka 1933, serikali ikaamua kusimaisha matumiz ya noti za shillingi 1000 ingawa zile za shillingi 10,00 ziliendelea. Wakati wa utawala mfupi wa Mfalme Edward wa nane mwaka 1936, hazikutolewa noti zozote. Noti nyingine zilitolewa wakati wa utawala wa mfame George wa sita (1936-1952), ambapo noti ya Shillingi 1 ilianzishwa. Noti hizo zilikuwa kama ifuatavyo.

1 EA Shilling

[​IMG]


5 EA Shilling

[​IMG]


10 EA Shilling

[​IMG][/​


20 EA Shilling

[​IMG][/​


100 EA Shilling

[​IMG][/​


Kutokana na uhadimu wake, sikuweza kupata noti za Shillingi 10,000. Hata hivyo miaka 11 ndani ya utawala wa mfalme George wa sita, iliamuliwa kufuta noti hizi za Shillingi 10,000 ambazo zilikuwa hazitumiki sana.

Baada ya kifo cha Mfalme George wa sita mwaka 1952 na binti yake Malkia Elizabeth wa pili kuchukua usukani noti zilizotolewa zilikuwa zinafanana na zile zilizokuwapo mwazoni isipokuwa aliondoa noti ya Shillingi 1 kwenye mzunguko.

5 EA Shilling

[​IMG]


10 EA Shilling

[​IMG]


20 EA Shilling

[​IMG]


100 EA Shilling

[​IMG]

2 comments: